Wednesday, February 22, 2012

MUUZA DVD KAMA AL-SHABAAB AU BOKO-HARAM

Huyu si Al-Shabaab wala Boko-Haram, la hasha, ni kijana Idrissa Sadiki Nyambo mkazi wa Mabibo Hostel, jijini Dar es Salaam ambaye ameamua kutoka na ‘staili’ ya aina yake ya kufanya biashara yake ya kuuza dvd.

Idrissa anasema kuwa ‘staili yake hiyo imemfanya apate wateja wengi kwa muda mfupi kwani wateja hao hutaka kujua anabeba vitu gani vya ziada na kwa nini avae hivyo. Ndipo hapo wanapojikuta wamenasa na kuanza kununua dvd zake.


Ustadh Idrissa Sadiki Nyambo akipita kutafuta wanunuzi

Anasema kuwa kwa siku mauzo yake hufikia 50,000/- na wakati mwingine hadi 80,000/-.

Huu ndiyo ubunifu ambao Idrissa Sadiki ameufanya na kujikuta maisha yake yanamwendea vizuri.


Mdau akichagua dvd kwa Ustadh Idrissa Sadiki Nyambo

No comments:

Post a Comment