Wednesday, February 22, 2012

MAUAJI SONGEA YAFIKIA WATU 10, FFU WAFYATUA RISASI NA MABOMU KUTAWANYA MAANDAMANO


Askari wa kutuliza ghasia (FFU) wakiondoa mkokoteni uliowekwa barabarani na vijana walioandamana katika eneo la lizaboni Manispaa ya Songea.


FFU wakiondoa magogo yaliyowekwa barabarani na vijana wa lizaboni kupinga wenzao kuuawa na watu wasiojuklikana katika maeneo mbalimbali mjini Songea.


FFU wakiwa na mmoja kati ya vijana aliyeshiriki maandamano haramu mjini Songea kupinga mauaji ya raia yanayoendelea mjini humo ambapo hadi sasa watu 10 wameshauawa na watu wasiojulikana.


FFU wakimshikilia mmmoja wa vijana waliokuwa wakiwarushia mawe katika mapambano kati ya polisi na baadhi ya wakazi wa Songea.


FFU wakiwa na vijana walioshiriki maandamano haramu katika manispaa ya songea kupinga mauaji ya wenzao hasa madereva wa pikpiki yanayoendelea mjini humo.


Mkuu wa Wilaya ya Songea ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo Thomas Sabaya akizungumza wakatika wa kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa ruvuma kushoto ni Mkuu wa mkoa huo Said Mwambungu.


Wajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Ruvuma wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo, Said Mwambungu (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichokaa baada ya kutokea mauaj ya vijana 3 na maandamano kati ya FFU na vijana hao.


Watendaji wa mitaa na Wenyeviti wao wakiwa katika mkutano ulioitishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Said Mwambungu wakati wa kikao cha dharura kujadili namna ya kukomesha mauaji ya watu wasio na hatia yanayoendelea katika manispaa ya Songea.

SOURCE: MUHIDINI AMRI/ SONGEA

No comments:

Post a Comment