Wednesday, February 22, 2012

MBABE ANAPOKUTANA NA MBABE MWENZIE..

Hii ilikuwa mitaa ya Ubungo Riverside jirani na darajani, jamaa anayedaiwa kuwa mbabe wa kuzuia watu kupita njia alipopewa 'kibano' cha haja na mbabe mwenzie baada ya kukerwa na vitendo vyake.

Kamera ya blogu hii ilipofika eneo hilo ilikuta mtifuano huo ambao ulianza kama muvi vile. Jamaa huyo ambaye jina lake halikuweza kupatika mara moja alikuwa akiwazuia watu kupita kwenye 'kamlango' kanakounganisha wakazi wa Ubungo Maziwa na Riverside.

Inadaiwa jamaa huyo alikuwa akimzuia kila anayepita hapo kwa kudai lazima kwanza atandikwe ngumi mbili au tatu hivi (yaani mpitanjia amtandike huyo jamaa) mpaka atakotosheka ndipo amruhusu. Ni jambo la kushangaza kwa kweli, lakini imetokea.

Baadaye vurugu iliibuka baada ya mmoja wa wapitanjia hao kukataa na ndipo 'mbabe' huyo akaanzisha vurugu kabla hajatiwa nguvuni na mbabe mwenzie.

Shuhudia tukio hilo katika picha zifuatazo;


Mbabe (kushoto) akimchimba mkwara mpitanjia sipite kwenye mlango huo


Mbabe mwenzie anatokea na kumtia nguvuni


Mbabe anatiwa nguvuni


Hapa ni kama anamwambia 'ukifurukuta nakutandika ngumi'

source: akidasenior

No comments:

Post a Comment