Friday, February 24, 2012

SUMBAWANGA YAZINDUA KAMPENI YA USAFI ‘SUMBAWANGA NG’ARA’


MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya akimwongoza Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal katika eneo la mkutano wa hadhara mjini Sumbawanga ambapo alisalimiana na wananchi na badaye alizindua kampeni ya kuuweka safi mji wa Sumbawanga iitwayo 'Sumbawanga ng'ara".


Mama Asha Bilal akimsalimia mtoto Juma Kapele(08) mlemavu wa ngozi 'albino' alipotembelea kituo cha kulelea watotot yatima kinachomilikiwa na kanisa katoliki cha Mtakatifu Martin de Pore kilichpo katika eneo la Katandala mjini Sumbawanga, mtoto Juma alipokelewa mawaka jana na kituo hicho baada ya kutoroshwa na mtu ikidaiwa kwa imani za kishirikina ambapo baada ya siku tatu aliokotwa porini akiwa ametelekezwa lakini alikuwa amepingwa chale mwili mzima


MKuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya akimkabidhi vifaa vya usafi Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal ili naye awakabidhi kikundi kinachofanya usafi katika mjini huo wa Sumbawanga muda mfupi kabla dk Bilal hajazindua kampeni ya usafi maarufu kama "Sumbawanga ng'ara"

source: Peti Siyame

No comments:

Post a Comment