Thursday, February 23, 2012

MAN U YAPIGWA 2-1 NA AJAX NYUMBANI


Mchezaji wa Manchester United, Phil Jones (kushoto) akiwania mpira na Aras Ozbiliz wa Ajax katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya raundi ya 32 uliochezwa kwenye Uwanja wa Old Trafford mjini Manchester usiku huu.

Ozbiliz aliisawazisha goli timu yake ya Ajax Amsterdam dakika ya 37 baada ya Hernandez kuifungia timu yake ya Manchester United goli la kuongoza katika dakika ya 6 ya kipindi ch kwanza.


Alderweireld akaongeza bao la ushindi dhidi ya timu yake ya Ajax katika dakika ya 87 ya kipindi cha pili cha mchezo na mpaka dakika 92 za mchezo kuisha Ajax walitoka vifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Manchester United.

Manchester United ilishindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford wakati wa mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulya (UEFA) iliyomalizika hivi punde.

Source: eurosport

No comments:

Post a Comment