Tuesday, January 26, 2010

TRA YAWAPIGA MSASA WA FORODHA NA USHURU WAFANYABIASHARA WAKUBWA

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kitengo cha Forodha na Ushuru leo kimeendesha warsha ya siku moja ya Mafunzo kwa wafanyabiashara wakubwa juu ya Ushuru wa Forodha.



Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Mamlaka hiyo, Walid Juma amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaandaa wafanyabiashara hao kuweza kuingia vema katika soko la pamoja la Afrika Mashariki pamoja na kuweza kupenya katika Soko la Kimataifa.

No comments:

Post a Comment