Tuesday, January 19, 2010

WATANZANIA WASISITIZWA UMUHIMU WA KUJENGA VYOO NA KUVITUNZA

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Prof. David Mwakyusa amewataka wananchi kujenga utamaduni wa kutumia vyoo safi na salama ili kujikinga na magonjwa ya milipuko.

Mwakyusa alitoa rai hiyo wakati wa sherehe ya kuhitimisha Kampeni ya 'Fyatua Choo Ushinde' iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo asubuhi.

"Tujenge utamaduni wa kutumia vyoo safi na salama ili kuepuka magonjwa ya milipuko." Alisema

Kampeni hiyo iliyoanza mwanzoni mwa mwaka huu imehitimishwa leo ambapo washindi kadhaa walikabidhiwa zawadi zao.


Waziri Mwakyusa akiangalia baadhi ya picha za vyoo

Mjomba Mrisho Mpoto akishangilia jambo na wanafunzi wakati wa sherehe hizo

No comments:

Post a Comment