Monday, March 23, 2009

BAA TANO ZATINGA FAINALI NYAMA CHOMA

Baa tano hapa jijini zimefanikiwa kutinga katika fainali ya shindano la Nyama choma na Safari Lager.

Akizitaja baa hizo, Meneja Mkuu wa bia ya safari, Fimbo Butala amesema kuwa ni pamoja Titanic iliyopo Vingunguti, Kisuma ya Temeke, Nguruko ya Mbezi beach, Africentre ya Ilala pamoja na Madrid Pub ya Tegeta.

Mwishoni mwa wiki hii kunatarajiwa kufanyika kwa fainali hizo katika Viwanja vya Leaders.


Meneja wa bia ya Safari, Fimbo Butala (kushoto) akifafanua jambo

No comments:

Post a Comment