Thursday, March 19, 2009

DUH! MGAMBO KUTOKA WAMACHINGA MPAKA BAA...

Katika hali ya kushangaza Kamera yangu ya 'Sponsor' iliwanasa mgambo wa jiji wakiwa wamevamia katika baa moja ya 'Honey Pub' eneo la Sinza Makaburini, na kulumbana na wahudumu kutokana na kilichoelezwa kuwa walikuta wateja wakinywa pombe muda ambao Serikali imepiga marufuku.

Baada ya malumbano yaliyochukua takribani saa nzima, ghafla nilishuhudia mgambo wale wakisomba baadhi ya viti vya wateja, kwa madai kuwa muhusika wa 'kaunta' waliyekuwa wakimuhitaji hakuwepo.

Chini ni picha mbalimbali za mgambo hao wakiwa katika eneo la tukio....


hapa walikuwa wakihesabu viti ili waondoke navyo


wakati wengine wakiendelea na zoesi la kuhesabu, huku wengine walikuwa na kazi na wamachinga wa cd waliokutwa katika baa hiyo...


baada ya kuvihesabu wanaondoka navyo sasa...

No comments:

Post a Comment