Monday, March 2, 2009

Picha za JK na ziara ya Bandarini..


Umesikia mzee wangu, hebu fanyeni maarifa haya makontena hapa yapungue... vinginevyo huo baharini tutasabisha foleni kama ya barabara ya Morogoro..



Vipi ndugu yangu, mbona unaniangusha kaka... hizi shehena zote hapa za nini?



...Haya mambo mzee yanahitaji uwajibikaji na si blaa blaa tu... fanyeni kazi jamani... Meli zinashindwa kushusha makontena hapa kisa nini...



'Umesikia ndugu yangu wa TICTS, hizi kontena hapa zinatakiwa kupungua... sio mnakalia blaa blaa tu nyingi sawa?



Hapa Rais Kikwete alikuwa akifafanua jambo kwa mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe (kushoto) kuhusiana na mlundikano wa shehena za kontena bandarini hapo... Kulia ni Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jason Rugaihuruza...



No comments:

Post a Comment