Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dustan Mrutu, alisema pamoja na kwamba bado Tanzania haijaathirika na mtikisiko huo, lakini dalili zinaonyesha kuwa nayo itaathirika hasa katika upande wa uchumi, biashara na chakula.
“Mtikisiko huu wa kiuchumi umeathiri sana uchumi wa nchi zilizoendelea hali ambayo pia inahatarisha uchumi wetu kwani mazao yetu kama pamba, kahawa na korosho soko litapungua,” alisema.
-Halima Mlacha-
Katibu Mtendaji wa TNBC, Dunstan Mrutu..
No comments:
Post a Comment