Wednesday, March 11, 2009

Kinyozi alamba dume TIGO...

Mkazi wa Vingunguti, Dar es Salaam ambaye ni fundi kinyozi, Christopher Damian ameibuka kidedea kwa kunyakua shilingi milioni 3.8/- za promosheni ya mapenzi ya kampuni ya simu za mkononi, Tigo, Dar es Salaam leo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha hizo, Christopher amesem "Sifikirii kufanyia chochote kwa sasa. Kwani sikutegemea kama nitashinda." Alisema.

Washindi wengine wanne waliojinyakulia zawadi mbalimbali ni pamoja na Elpidius Katema na Mohammed Ali ambao wamejinyakulia Ipod. Wengine ni Bruno Mulokozi pamoja na Edwin Kajuna ambao wameshinda simu za mkononi mpya za nokia 6300.


Christopher Damian 'fundi kinyozi' akionyesha mapesa yake aliyolamba toka Tigo...

No comments:

Post a Comment