Monday, March 16, 2009

HOFU YATAWALA MUSWADA MPYA WA SHERIA YA WANYAMAPORI AFRIKA MASHARIKI..

Muswada wa sheria ya wanyamapori na utalii wa bunge la Afrika Mashariki unatarajiwa kupelekwa Bungeni, baada ya wadau mbalimbali wa sekta hiyo kutoa maoni yao na michango mbalimbali juu ya muswada huo, jijini Dar es leo mchana...

Miongoni mwa maoni yaliyotolewa na wadau ni pamoja na suala la ushindani wa kibiashara, tatizo la lugha ya mawasiliano, na mengine mengi ambapo wamesema muswada huo utakapopitishwa utaleta changamoto kwa nchi ambazo hazijajitangaza zaidi katika Utalii.

Miongoni mwa nchi hizo walizozitaja ni pamoja na Tanzania, Rwanda na Burundi.


Mwenyekiti wa kamati ya Kilimo na Utalii ya Bunge la Afrika Mashariki, Dk. George Nangale akionyesha muswada wa sheria mpya kwa wadau leo jijini..

No comments:

Post a Comment