Thursday, March 19, 2009

TLP KUMEKUCHA....

Chama cha siasa cha Tanzania Labour (TLP), leo kimetoa fursa kwa wananchama wake wawili kuchukua fomu za kugombea nafasi ya Uenyekiti ambayo kwa sasa bado inashikiliwa na Agustino Lyatonga Mrema.

Joram Kinanda ambaye ni Mkurugenzi wa Kampeni na Uchaguzi wa TLP anasema "Ni muda muafaka sasa mheshimiwa Mrema kung'atuka atuachie na sisi nafasi za kukiongoza Chama."

Naye Katibu Mwenezi wa chama hicho, Benedicto Mutungirehi amelalamikia kitendo cha kutenguliwa ujumbe wa kukiwakilisha chama hicho katika vikao vya Kituo cha Sheria nchini -TCD, na kusema kuwa hizo ni njama dhidi yake za kumkatisha tamaa katika uchaguzi.


Katibu Mkuu Taifa wa TLP John Komba (kulia) akikabidhi fomu kwa Joram Kinanda

No comments:

Post a Comment