Monday, March 9, 2009

WANAJESHI ZAIDI 12,000 WA MAREKANI KUONDOKA IRAQ...

Wanajeshi 12,000 wa Marekani waliopo Baghdad, Iraq wanatarajiwa kuondolewa ifikapo mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, limesema jeshi la Mrekani.

Uondoshaji wa Askari hao mjini Baghdad unafuatia Jeshi la Marekani kuondosha zana zake zaidi nchini humo na kuzirejesha Marekani, Alisema Meja Jenerali David Perkins ambaye ni Msemaji wa Jeshi hilo, wakati wa mkutano na waandishi wa habari pamoja na Msemaji wa Serikali ya
Iraqi, Ali al-Dabbagh.

Perkins alisema wanajeshi hao wataondolewa kuanzia brigedi 14 na 12.

Ijumaa, Rais wa Marekani Barack Obama alitangaza mpango wa kuondoa vikosi zaidi nchini Iraqi mpaka mwishoni mwa mwezi Agosti na kubakisha idadi ya wanajeshi 35,000 mpaka 50,000O ya idadi ya sasa ambayo inafikia 140,000.


Baadhi ya wanajeshi wa Marekani wakiwa katika mitaa ya Baghdad

No comments:

Post a Comment