Monday, March 9, 2009

WAKILI ATUHUMIWA KUIIBIA BARCLAYS

POLISI Jijini Dar es Salaam inamshikilia mwanasheria wa kujitegemea Theonest Rutashoborwa (44) kwaajili ya mahojiano kuhusiana na tuhuma za kuiibia benki ya Barclays.

Rutashoborwa ambaye anatoka katika kampuni ya wanasheria ya Briliance Law Chamber, anashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tuhuma za kula njama ,kughushi na kuiibia benki ya Barclays Dola za Kimarekani 1,081,263.

Alisema mwanasheria huyo anahojiwa kama mtu mwingine anavyohojiwa hivyo endapo atadhibitika kula njama, kughushi kwa aina yoyote ile ataungwanishwa na washtakiwa wengine ambao tayari wameshafikishwa mahakamani kuhusuana na tuhuma hizo.

“Kesi inapofika mahakamani si kwamba uchunguzi wake hauendelei hivyo tunafanya mahojiano na Rutashoborwa ili kubaini kama amehusika na tuhuma hizo au la , endapo atabainika kuhusika sheria itachukua mkondo wake na kama hakuhusika basi lakini si kwasababu ni mwanasheria hawezi kuhojiwa la bali polisi inafanya mahojiano na mtu yoyote yule”.

No comments:

Post a Comment