Tuesday, March 10, 2009

MWINYI ASISITIZA UPENDO NA AMANI...

Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi amewataka waumini wa dini zote hususan waislamu na wakristo nchini kudumisha upenda na amani ili kuendelea kuwa na taifa la amani duniani.

Mwinyi alisema hayo wakati wa sherehe za mkesha wa sikukuu ya Maulid zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

"Niseme tu, tuendeleze upendo, amani na mshikamano miongoni kwa waumini wa dini zote nchini." Alisema.

Sherehe za mkesha wa sikukuu ya Maulid zilifanyika usiku wa kuamkoa leo katika Viwanja vya Mnazi mmoja, Dar es Salaam na kuhudhuruiwa na viongozi mbalimbali wa dini ya kiislam, akiwemo Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Issa Shaaban Bin Simba, Kaimu Mufti Suleyman Gorogosi, Sharif Hussein Badawiy, pamoja na masheikh wakuu toka mikoa mbalimbali.

PICHA ZA MKESHA WA MAULID, VIWANJA VYA MNAZI MMOJA...


Madrasatul Hidaya katika dufu...


Waumini wamehamasika na dufu wallaah!


Sheikh Mwinyi na Sheikh Gorogosi katika tabasamu...


Sheikh Mohammed Kisenga wa Handeni Tanga akisoma mlango wa 4 kwa mbwembwe...


Kila mtu na pozi lake, mradi burudani... we acha tu!

No comments:

Post a Comment